POLISI WAZUIA MKUTANO WA ZITTO KABWE TANGA


Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga  limezuia mkutano wa ndani wa Kiongozi wa Chama wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe wa uzinduzi wa matawi kutokana na kuwapo   vurugu.

Hatua hiyo ilitokana na taarifa za  intelijensia ambazo zilidai kutokea   vurugu ambazo ziliratibiwa na wanachama na wafuasi wa Chama cha CUF.

Akizungumza hali hiyo jana, Kiongozi wa   ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema   vitendo vinavyofanywa na vyombo vya dola vya kuzuia shughuli za chama hicho vinaonyesha namna ambavyo kinahofiwa kwa kuwa na nguvu kubwa kwa umma.

Alisema zuio hilo linaonyesha namna wanavyoingizwa kwenye mitego ya wanachama wao waonekane wanafanya vurugu.

Ziito alidai   kumekuwa na mazuio ya kila mara kwa chama hicho   kinapojaribu kufanya shughuli zake kama vile mikutano ya ndani ya kuimarisha uhai wa chama .

Hata hivyo kiongozi huyo alishangazwa na jeshi hilo kuruhusu vyama vingine kama CUF na CCM kuendelea kufanya mikutano ya ndani na hadhara bila ya vizuizi vya aina yoyote ile.

Alisema   mpaka jana Jeshi la Polisi Wilaya ya Tanga, lilikuwa limetoa kibali kwa chama hicho kuendelea kufanya shughuli zake ikiwamo kupokea wanachama wapya na mikutano ya ndani kabla ya kuzuia shughuli hizo.

Akizungumzia hali zuio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, alisema   taarifa za  intelejensia zinaonyesha   iwapo chama hicho kitaruhusiwa kufanya shughuli zake kunaweza kutokea uvunjifu wa amani.

Alisema   kutokana na uchunguzi wao walibaini  baada ya kuwapo   mivutano ya  siasa baina ya chama hicho na CUF  kutokana na kunyang’anyana ofisi na kuharibu baadhi ya thamani za ofisi hizo jambo linaloweza kusababisha kutokea   vurugu na amani kutoweka.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527