NAPE AFUNGUKA TENA TUKIO LA KUTISHIWA BASTOLA


Mbunge wa Mtama,Nape Nnauye amezungumzia kwa mara ya kwanza tukio lake la kutishiwa bastola miaka miwili iliyopita.

Katika maelezo yake, Nape amsema wakati anatishiwa kwa bastola miaka miwili iliyopita  walikuwapo watu mbalimbali akiwamo Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD)pamoja na Kamanda wa polisi wa Mkoa (RPC).

Pamoja na hayo alishangaa tukio lake hilo kutotolewa ufafanuzi wowote na Serikali wakati inalijua vizuri.

Nape aliyasema haya bungeni wakati Bunge lilipokaa kama Kamati ya Matumizi kujadili bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Aidha Nape aliitaka Serikali ijitenge na matukio ya kihalifu kama ya tukio lake kwa kuwa anaamini aliyemtishia hakutumwa na Serikali ingawa anamfahamu vizuri.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527