MAKAMU WA RAIS KUFUNGUA KONGAMANO LA PILI LA MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA HAYATI SHEIKH ABEID AMANI KARUME LEO


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi tarehe 4, Aprili 2019 atakuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Pili la Maadhimisho ya kumbukumbu ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Kwanza wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume. 

Mada kuu ya Kongamano hili ni “Uhai wa Fikra za Falsafa za Abeid Amani Karume katika Zanzibar ya leo”.

Kongamano hilo limeandaliwa na Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na litafanyika kwenye Kampasi ya Zanzibar Bubu ambapo baada ya Makamu wa Rais kufungua Kongamano hilo atatunuku zawadi kwa washindi wa Insha.

Aidha baada ya ufunguzi kutaendeshwa mada mbali mbali zitakazotolewa na Mhe.Dkt. Saada Mkuya Salum na Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud

Imetolewa na:
Ofisi ya Makamu wa Rais
Zanzibar


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post