BABA AUA MTOTO KWA KUMNYONGA AKIDAI 'AMEBAMBIKIZIWA'


Jeshi la Polisi mkoani Pwani linamshikilia mkazi wa mtaa wa Vitendo katika kata ya Misugusugu wilayani Kibaha, Pwani, Robison Ernest (33) kwa tuhuma za kumwua kwa kumnyonga mtoto wake wa Modesta Robison miezi sita akidai kuwa si mwanae.

Inadaiwa kuwa Ernest ambaye ni fundi ujenzi alifanya kitendo hicho cha kinyama wakati mama wa mtoto huyo akiwa sokoni kwa ajili ya kununua mahitaji ya nyumbani.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amesema kuwa baada ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho, aliuficha mwili chini ya uvungu wa kitanda kisha huku baba huyo akihamia chumba kingine.

Akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha leo Jumanne (Aprili 2, 2019), Kamanda Nyigesa alisema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili Mosi, mwaka huu majira ya saa 4:30 asubuhi kwenye mtaa huo.

Na John Gagarini- Habarileo 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527