HAJI MANARA ATAJA TOFAUTI YA KOCHA WA SIMBA NA YANGA


Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara, ametaja utofauti wa makocha Mwinyi Zahera wa Yanga na Patrick Aussems wa Simba.

"Tofauti ya kocha wa mpira na kocha wa Sunsumia au kibao kata unafungwa unawapongeza wa shindi na kukubali mapungufu yako angekuwa yeye!!!

Waamuzi wanatuonea mimi nimefundisha ulaya mika Arobaini (Ukigogle huoni timu alizo fundisha zaidi ya kufundisha kucheza Ndombolo na Mayenda) oooh Simba inabebwa leo Fei Toto hawakuvaa boksa na hawajala toka juzi!!!

"Ila akishinda sasa ninafuu kupiga gitaa kuliko Diblo na ile fasi ya putuluu imekuja na Ndege na ndio mana sisi wa Congo tunapendwa na madada wa kibongo .

Kocha mzuri huzungumzia vitu Technical na sio Riwaya kwa mahawala wako wanao tumia mkorogo wa buku" ameandika Manara kupitia ukurasa wake wa Instagram.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527