BABA DIAMOND AOMBA KOLABO NA WANAWE


Baada  ya baba mzazi wa Diamond Platnumz, Mzee Abdul Jumaa kuachia wimbo wake mpya ambao ameshirikisha na Sungura amefunguka kuwa amefanya ngoma hiyo bila gharama yoyote na anafurahi kwa sababu wananchi wameupokea vizuri.

Baba Diamond alisema ngoma yake hiyo aliyoipa jina la ‘Dudu la Yuyu’ itakuwa ni ngoma yake ya mwisho labda kama atashirikishwa na watoto wake (Diamond au Queen Darleen), basi ataimba kwa sababu anajua.

Mbali na hapo amemshukuru Diamond kwa kusapoti kazi yake na kuwa amefurahi sana kwa hicho kitendo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527