ZAHERA AONDOKA..AOMBA ASIULIZWE CHOCHOTE


Kocha Mwinyi Zahera akiwa na wachezaji wa Yanga.

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera baada ya mchezo wa jana dhidi ya KMC ambapo Yanga ilishinda mabao 2-1, ameaga kuwa anaondoka nchini kuelekea kwao DR Congo.

Zahera anakwenda DR Congo kwaajili ya majukumu ya timu ya taifa ambayo yeye ni kocha msaidizi huku akisisitiza kuwa taifa lake lina mchezo mgumu sana dhidi ya Liberia kuwania kufuzu AFCON 2019.

''Naenda Congo, tupo na mechi ngumu sana, nisiulizwe chochote kuhusu Simba au Yanga nawaachia namba ya kocha msaidizi Noel Mwadila mtamuuliza yote mimi sitamjibu hata mtu mmoja'', amesema.

Zahera anaondoka nchini kesho Jumanne Machi 3, 2019, lakini hajaweka wazi kama anaondoka na mshambuliaji Heritier Makambo ambaye alitajwa katika kikosi cha wachezaji 40 wa awali kuelekea mchezo huo.

DR Congo ipo kundi G ambalo linaongozwa na Zimbabwe yenye pointi 8, Liberia yenye pointi 7 huku DR Congo wakiwa na pointi 6 wakati Congo Brazzaville wakiwa na pointi 5.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527