WAZIRI AAGIZA WANASIASA WAHUNI WANAOMTUKANA RAIS MAGUFULI WAKAMATWE


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola ameagiza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa wanasiasa ambao wanafanya mikutano ya ndani ambayo imepigwa marufuku.

Kangi Lugola ametoa kauli hiyo akiwa Mkoani Morogoro wakati akizungumza na wananchi wa Mjini Kilosa ambapo amesema ana taarifa za kuwepo kwa baadhi ya wanasiasa wa upinzani wanaofanya vikao vyao vya ndani huku wakitoa kauli ambazo zinaashiria uchochezi.

“Mimi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sitakubaliana na kiongozi wa chama chochote kuvunja agizo tulilolitoa nchi nzima kwa kutoruhusu kufanyika mikutano ya hadhara ya siasa, na pia kupitia mikutano ya ndani ambayo inafanyika, baadhi ya wanasiasa wahuni wanamtukana Rais ambaye ndiyo kiongozi Mkuu wa nchi, mimi sitakubaliana na hilo,” amesema Lugola.

Aidha Lugola amesema Rais Magufuli ni kiongozi ambaye kwa muda mfupi ameiletea mabadiliko makubwa nchi na pia ana mipango mikubwa ya maendeleo yanayokuja katika uongozi wake.
Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527