MAMA AJIFUNGUA WATOTO WATANO KWA MKUPUO

Mama aitwaye Evelyn Namukhula mwenye umri wa miaka 28  amejifungua salama watoto watano katika Hospitali Kuu ya Kakamega nchini Kenya

Evelyn Namukhula  amejifungua kupitia njia ya upasuaji, ambapo madaktari wamethibitisha hali ya afya ya watoto wake ni nzuri. 

Amejifungua wasichana watatu na wavulana wawili. 

Kabla ya kujifungua, Namukhula alikuwa na watoto wanne anaoishi nao na baba yao Herbert Nabwire katika kijiji cha Sisokhe, eneo bunge la Navakholo.

 "Namshukuru Mungu kwa mujiza huu. Hata hivyo, nawaomba wahisani kujitokeza kwa kuwa sitakuwa na uwezo wa kuwalea pekee yangu," alisema. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527