Picha : TIMU YA WAKONGWE 'SHYTOWN VETERAN SPORTS CLUB' YAZINDULIWA RASMI UWANJA WA CCM KAMBARAGE

Timu ya wakongwe (Shytown Veteran Sports Club) imezinduliwa rasmi kwenye Uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga Mjini, kwa kufanya Bonanza la michezo ambalo limeshirikisha timu za wakongwe kutoka mikoa mitatu Tabora, Simiyu pamoja na wenyeji Shinyanga Veteran.


Uzinduzi huo umefanyika leo, Machi 31,2019 kwenye uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao.

Akizungumza, Mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa timu hiyo ya Shytown Veteran, Afisa Tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akimwakilisha mkuu wa wilaya hiyo Jasinta Mboneko, alisema Serikali itashirikiana bega kwa bega na timu hiyo ikiwemo kutatua changamoto ambazo zinawakabili.

“Mkuu wa wilaya ya Shinyanga amenituma kuwaletea salamu zake kuwa michezo ni mazoezi na inainua vipaji, hivyo ameahidi Serikali itashirikiana nanyi kikamilifu katika kuhakikisha mnayafikia malengo yenu,”alisema Beda.

“Hivyo kwa kuunga mkono nami natoa mipira miwili kwenye Timu hii ya Shtown Veteran Sports Club ambayo mtakuwa mkiitumia kwenye michezo yenu, ambapo nawaomba pia mpange siku ili mje kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya tupate kuzungumza kwa pamoja ili kupanga mikakati dhidi ya timu yenu,”aliongeza.

Naye Katibu mkuu wa timu hiyo Mohamed Katoto akisoma Risala kwa mgeni huyo rasmi, alisema Timu hiyo waliiunda Machi 23,2018 na kupata usajili kutoka kwenye Baraza la Michezo Novemba 20,2018, ambapo leo ndiyo wameamua kuizindua rasmi ikiwa na wanachama 55.

Alisema changamoto ambayo inawakabili kwa sasa ni ukosefu wa fedha za kuendeshea Timu hiyo kutokana na kutopata wadhamini, ambapo wameomba wajitokeze kuwafadhili ili kutoa hamasa kwenye timu za wakongwe.

Aidha kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao ambaye naye amehudhuria uzinduzi huo wa Timu ya Shytown Veteran, amewapongeza wakongwe hao kwa kuunda Timu hiyo na kuahidi kuwapatia mipira miwili.

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Mgeni Rasmi Afisa tawala wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akimwakilisha mkuu wa wilaya hiyo Jasinta Mboneko kwenye uzinduzi wa Timu ya wakongwe Shytown Veteran Sports Club, kwa kupiga mkwaju wa Penati ambao ulimshinda Golikipa wa timu hiyo ya Shytown Veteran. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog

Afisa Tawala wilaya ya Shinyanga Kamara Beda, akizungumza kwenye uzinduzi wa timu ya Shytown Veteran Sports Club na kuahidi Serikali itashirikiana nao kikamilifu kwa kutatua baadhi ya changamoto ambazo zinawakabili.

Katibu mkuu wa timu ya Shytown Veteran Sports Club Mohamed Katoto akisoma risala ya timu hiyo na kueleza changamoto ambazo zinawakabili ambazo ni ukosefu wa fedha za kuendeshea timu, ukosefu wa kiwanja pamoja na vifaa vya michezo, na kuomba wafadhili wajitokeza kuwekeza kwenye timu hiyo.

Mwenyekiti wa timu ya Shytown Veteran Sports Club Christopher Msigwa akitoa shukrani kwa viongozi kujitokeza kuahidi kuisaidia timu hiyo pamoja na kutoa ahadi ya kuipatia mipira.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao, akitoa pongezi ya kuanzishwa kwa timu hiyo ya wakongwe Shytown Veteran Sports Club na kuahidi kutoa zawadi ya mipira miwili.

Diwani wa Kata ya Kambarage manispaa ya Shinyanga Hassan Mwendapole mahali ambapo uwanja huo wa michezo upo kwenye Kata yake akitoa ahadi ya kutoa mpira mmoja kwa timu hiyo ya Shytown Veteran Sports Club.

Katibu mkuu wa timu ya Shytown Veteran Mohamed Katoto akishikana mikopo na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao mara baada ya kumaliza kusoma risala ya timu hiyo.

Mgeni Rasmi Afisa Tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akishikana mikono na wachezaji wa timu ya Shytown Veteran Sports Club tayari kwa ufunguzi wa bonanza hilo la michezo.

Utoaji wa salamu ukiendelea kwa mgeni rasmi.

Mgeni rasmi akitoa salamu kwa timu ya Busulwa Veteran ambayo kwa ajili ya mchezo dhidi ya Shytown Veteran kwa ufunguzi wa bonanza hilo la michezo la kuzindua rasmi timu hiyo ya Shytown Veteran Sports Club.

Mchezo ukichezwa kati ya Busulwa Veteran wenye Jezi ya Njano, pamoja na Shytown Veteran Sports Club ambao waliiubuka na ushindi wa magoli mawili yaliyofungwa na Mdee Aboo pamoja na Mohamed Katoto.

Mchezo ukiendelea kati ya Simiyu Veteran wenye Jezi ya blue pamoja na Unyanyembe Veteran ya Tabora ambapo walitoka suluhu ya kufungana goli moja kwa moja.

Mchezaji wa Simiyu Veteran akiwa chini akigangwa mara baada ya kukanywaga kwenye mchezo wao dhidi ya Unyanyembe Veteran ya Tabora.

Kabumbu likiendela kusakatwa kwenye uzinduzi wa timu ya Shytown Veteran Sports Club.

Shytown Veteran Sports Club wenye Jezi ya rangi ya machungwa, wakiwa na Unyanyembe Veteran ya Tabora, ambao waliibuka na ushindi wa goli Moja.

Kabumbu likiendelea kusakatwa kwenye uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga.

Wadau wa michezo pamoja na baadhi ya wachezaji wa timu ya Shytown Veteran Sports Club wakishuhudia Kandanda safi likiendelea kuchezwa kwenye uwanja wa CCM Kambarage.

Wadau wa michezo pamoja na baadhi ya wachezaji wa timu ya Shytown Veteran Sports Club wakishuhudia Kandanda safi likiendelea kuchezwa kwenye uwanja wa CCM Kambarage.

Awali Mgeni rasmi Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akisalimiana na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao kabla ya kuzindua bonanza la michezo la uzinduzi rasmi wa timu ya Shytown Veteran Sports Club.

Wachezaji wa timu ya Shytown Veteran wakipiga picha ya pamoja na mgeni rasmi Afisa Tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda, Diwani wa Kata ya Kambarage Hassan Mwendapole pamoja na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527