WAZIRI MKUU AWAHAMASISHA WATANZANIA KUISHANGILIA TAIFA STARS KESHO

Pichani ni Mheshimiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwahamashisha Watanzania kujitokeza kwa wingi kesho Jumapili Machi 24, kuishangilia Taifa Stars katika mchezo wake dhidi ya Timu ya taifa ya Uganda.

Matokeo ya ushindi dhidi ya Uganda yanaweza kuipa Stars nafasi ya kufuzu kwa fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika mwezi Juni nchini Misri.

Hata hivyo ili Stars iweze kufuzu lazima Cape Verde iifunge au itoke sare na Lesotho. Mchezo baina ya timu hizo utapigwa huko Cape Verde muda sawa na mchezo kati ya Stars dhidi ya Uganda utakaopigwa kesho saa 12 jioni

Wapinzani wa Stars, Uganda Cranes wanatarajiwa kuwasili nchini leo. Uganda iliweka kambi ya wiki moja nchini Misri kujiandaa na mchezo huo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527