RUFAA YA MBOWE,MATIKO KUSIKILIZWA KESHO

Mahakama Kuu ya Tanzania kesho Machi 6,2019 inatarajia kuanza kusikiliza rufaa ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko ya kupinga kufutiwa dhamana na Mahakama ya Kisutu.

Hatua hiyo inakuja baada ya Mahakama ya Rufani Tanzania kutupilia mbali pingamizi za Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ya kupinga mahakama hiyo kusikiliza rufaa hiyo, Machi 1, 2019.

Rufaa hiyo inatarajiwa kusikilizwa kesho mbele ya Jaji Sam Rumanyika ambapo alisimamisha kusikiliza rufaa hiyo kutokana na rufaa ya DPP.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527