ATOLEWA NJE YA NDEGE BAADA YA KUNASWA AKIOMBA 'MUNGU WAKE' WAPATE AJALI ANGANI


Mwanaume mmoja ametolewa kutoka kwenye ndege moja iliyokuwa ikisafiri kutoka Uwanja wa Ndege wa Islamabad nchini Pakistan kwenda Dubai, baada ya kufanya maombi akimuomba ‘mungu wake’ kusababisha ajali ya ndege hiyo.

Abiria huyo ambaye alitambuliwa kwa jina moja la Khalil alikuwa akisafiri kuelekea Australia kupitia Dubai, na imefahamika kuwa alianza kuomba maafa ya mauti yatokee punde tu alipoketi ndani ya ndege hiyo katika Uwanja wa Ndege.

Maombi yake yaliwafanya abiria kuhofia na kuanza kuingiwa na wasiwasi, hasa wasafiri na wahudumu wa ndege waliokuwapo.

Baada ya tukio hilo Rubani alitahadharisha idara ya ulinzi katika uwanja huo , na maafisa wa usalama walipofika wakamuondoa ndani ya ndege.

Chanzo - Daily Mail UK

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527