TAHARUKI YATANDA OFISI ZA CLOUDS KIFO CHA KIBONDE


 Kila mfanyakazi katika viunga vya ofisi za Clouds Media Group anaonekana kukumbwa na fadhaa. Ni ngumu kuamini kuwa ndani ya siku 10 wamepokea taarifa za msiba wa watu wawili muhimu kwao.

Mtangazaji Ephraim Kibonde amefariki siku nane baada ya Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa kampuni hiyo, Ruge Mutahaba kufariki Februari 26, 2019.

Katika ofisi za Clouds Media group, wafanyakazi wameonekana wamekaa kimafungu sehemu ya kuegesha magari kila mmoja akiwa na simanzi na wengine wakilia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527