CUF WAFANIKIWA KUIREJESHA OFISI YAO YA MAKAO MAKUU ZANZIBAR

Hatimae Chama cha wananchi CUF leo Jumanne Machi 26,2019 kimefanikiwa kudhibiti Makao makuu ya chama hicho yaliopo Mtendeni mjini Unguja na kupachika bendera zoezi ambalo lilisimamiwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la Polisi.

Zoezi hilo limeongozwa na mjumbe wa bodi ya wadhamini, Mussa Haji Kombo pamoja na wanachama wengine wa chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kombo amesema wamelazimika kuweka bendera wakifahamu kuwa ofisi hiyo ni miongoni mwa mali za chama hicho.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527