AFARIKI KWENYE DIMBWI LA MAJI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Thobias Sedeyoka, amethibitisha kutokea kwa vifo vya watu wawili kulikosababishwa na mvua kubwa za masika zilizoanza kunyesha visiwani humo.

Waliofariki dunia ni Hassan Mohamed (4) aliyezama kwenye dimbwi la maji ya mvua, na Skachi Abdallah Zahor (26) mkazi wa Kidongo Chekundu, baada ya kuanguka na pikipiki (bodaboda) aliyokuwa amepakiwa katika eneo la Mazizini mjini.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi amesema jitihada za polisi kumtafuta dereva wa bodaboda aliyehusika na ajali hiyo iliyosababisha kujeruhiwa Skachi Abdallah Zahor kwa zinaendelea na akipatikana atachukuliwa na hatua za kisheria.

Hivi karibuni mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa Zanzibar iliwataka wananchi na mamlaka husika kuchukuwa tahadhari kutokana na msimu wa mvua za masika kutarajiwa kuanza wakati wowote.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527