SIMBA YAPATA KOCHA MSAIDIZI

Hivi karibuni mwekezaji na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya klabu ya Simba Mohammed Dewji aliweka wazi kuwa tayari wameshatoa maelekezo kwa CEO wa Simba Crescentius Magori kuhakikisha timu inapata kocha msaidizi jambo ambalo limekamilika.

Nafasi hiyo iliyoachwa wazi mwanzo mwa msimu huu na aliyekuwa kocha msaidizi wa Simba Masoud Djuma, imezibwa na kocha mtanzania Denis Kitambi.

Kitambi amewahi kuzifundisha vilabu vya Ndanda FC akiwa kama kocha mkuu, Azam FC akiwa kocha msaidizi chini ya Stewart Hall ambaye pia alikwenda kufanya naye kazi kama kocha wake msaidizi katika klabu ya AFC Leopards ya Kenya.

Imeelezwa kuwa tayari amekwishajiunga na kambi ya timu hiyo jijini Dar es Salaam ambapo mchezo wake wa kwanza kukaa kwenye benchi la ufundi utakuwa ni dhidi ya Yanga Jumamosi hii.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527