MSANII NGULI WA FILAMU AFARIKI DUNIA


Msanii nguli wa filamu wa Marekani, Kristoff St. John (52) amefariki dunia baada ya mwili wake kukutwa nyumbani kwake huko San Francisco, usiku wa Februari 2, 2019.

Kristoff ambaye alishawahi kuwekwa kwenye hospitali ya watu wenye matatizo ya akili baada ya kujaribu kujiua kwa bunduki, alipata umaarufu mkubwa kwa kuigiza kwenye filamu, ambazo alianza kujihusisha nazo akiwa na miaka nane tu.

Mpaka sasa chanzo cha kifo chake hakijajulikana, ila polisi wa Francisco wameshuku huenda ikawa ni kuzidisha madawa, yaliyosababisha kifo chake.

Star huyo ameshawahi kuigiza kwenye filamu mbali mbali zikiwemo That’s My Mama, Wonder Woman, Roots, The Next Generation, na nyinginezo nyingi.

Star huyo hivi karibuni alimchumbia mchumba wake Kseniya Olegovna Mikhaleva, na walitarajia kufunga ndoa ndani ya mwaka huu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527