AUAWA KWA KUKATWA MAPANGA AKITETEA MIFUGO ISILE MAZAO YAKE

Mkazi wa Kijiji cha Makole aliyetambulika kwa jina moja la Ally ameuawa kwa kukatwa mapanga.


Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Edward Bukombe amethibitisha kutokea mauaji hayo yaliyofanyika kijiji cha Makole, Kata ya Kwalukonge wilayani Korogwe.

Kamanda Bukombe alisema mauaji hayo yalitokea baada ya mfugaji, Paulo Marko (24) kuingiza mifugo yake katika shamba la Ally, na katika mabishano, ndipo Marko aliamua kumkata mapanga hadi kufikwa na umauti.

“Ni kweli kumetokea mauaji katika Kijiji cha Makole, Kata ya Kwalukonge wilayani Korogwe ambapo mfugaji Paulo Marko amemuua bwana Ally wakati akitetea mazao yake,” alisema.

Aliongeza, “mfugaji aliingiza ng’ombe wake kwenye shamba la mkulima akaanza kula mazao na mkulima huyo alipomwambia aondoe ng’ombe wake, katika mabishano ya muda mrefu ndipo ikafikia hali hiyo ya mauaji.”

Via Habarileo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527