AMUUA MKEWE KWA KUMNYONGA AKIMTUHUMU KUCHEPUKA NA WANAUME WANAOMPA POMBE KAHAMA


Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Maselle Mheziwa (40) mkazi wa Kagongwa wilayani Kahama ameuawa kwa kunyongwa shingo na mmewe aitwaye Omary Juma (46),mkazi wa Kagongwa kutokana na ugomvi wa wivu wa kimapenzi.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao,tukio hilo limetokea Februari 2,2019 majira ya saa mbili asubuhi katika kata Kagongwa, tarafa ya Isaghehe, wilaya ya Kahama.

 "Chanzo ni ugomvi uliokuwepo kati ya marehemu na mumewe akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wengine kwa sababu ananunuliwa pombe na wanaume bila kibali kutoka kwa mmewe",amesema Kamanda Abwao.

"Mbinu iliyotumika ni kumnyonga shingo na kumweka njiani ili asijulikane. Mtuhumiwa amekamatwa kwa hatua zaidi za kisheria",ameongeza.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.


Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog


Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install


https://bit.ly/2Qb7qyF



NB: App uliyokuwa unatumia mwanzo tumeifuta na kuleta mpya ya kisasa zaidi..Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527