Picha : MAPACHA WAZUA GUMZO BAADA YA KUOA MWANAMKE MMOJA

 Mapacha wakiwa na mke wao

Mapacha wa kiume wamevunja rekodi nchini Afrika Kusini baada ya kufunga pingu za maisha na mwanamke mmoja.

 Ndugu hao wawili walipiga picha pamoja na mke wao huku wamevalia ngozi za chui. 

Mwanamke huyo alikuwa kati kati yao huku akiilaza mikono yake kila pande kwenye mapaja ya waume zake.

 Huku waume hao wakionyesha furaha kwa tabasamu kubwa, mwanamke huyo alionekana kama aliyechanganyikiwa.

Katika picha kadhaa zilizochapishwa katika mtandao wa Twitter na Catchvibe Moatshe, harusi hiyo iliyofanyika Jumamosi, Februari 2 iliwaacha wengi wakishangaa kuhusu jinsi ndugu hao wawili walikubaliana kumuoa mwanamke mmoja.

 Baadhi walikataa wakidai kuwa mke mmoja hawezi kukubali kuolewa na wanaume wawili.

 Walidai kuwa mume mwengine alikuwa nao kwa ajili ya picha tu wala si kwa ndoa. Suala hilo limesalia kuwa kitendawili, wengi wakijiuliza maswali bila majibu. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527