AKAMATWA AKISAFIRISHA MAITI YA MTOTO


Mwanaume mmoja anashikiliwa na vyombo vya usalama nchini Malawi baada ya kukutwa akisafiri na maiti ya mtoto kwenye treni.

Akithibitisha kukamatwa kwa mtu huyo, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini humo, Joseph Sauka, amesema kwamba mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la James Majawa, 28, wa kijiji cha Chimphamba alikuwa akisafiri kutoka Limbe kwenda Nayuchi.

Kamanda Sauka ameeleza kwamba maiti ya Mtoto huyo ilibainika baada ya harufu ya kitu kilichoharibika kuenea kwenye Treni hiyo iliyokuwa na abiria wengine.

Amefafanua kwamba baada ya upekuzi ndipo maiti hiyo ikabainika huku ikiwa imetolewa sehemu za siri.

Hata hivyo Kamanda Sauka ameeleza kwamba bado wanaendelea na uchunguzi zaidi huku wakisisitiza kwamba maiti hiyo siyo ya mtoto mwenye ualbino.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527