RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MWINGINE


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amefanya uteuzi wa Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Taifa kwa watu wenye ulemavu na Mwenyekiti wa wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA).

Walioteuliwa kushika nyadhifa hizo ni Dkt. Lucas Luhende Kija ambaye atakuwa mwenyekiti wa baraza la ushauri la taifa kwa watu wenye ulemavu akitokea chuo kikuu kishirikishi cha elimu (DUCE) ambapo alikuwa Mhadhiri.

Mwenyekiti mpya wa bodi ya REA ni Dkt. Michael Pius Nyagoga ambaye awali alikuwa kamishna msaidizi wa Sera, Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha na Mipango.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imesema kuwa uteuzi huo umeanza tarehe 13, Februari 2019.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527