ASHUSHIWA KICHAPO BAADA YA KUGOMA KUFANYA MAPENZI NA MMEWE KINYUME NA MAUMBILE

Mwanamke mmoja mkazi wa Kijichi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, anadai kupigwa na kujeruhiwa usoni ambako ameshonwa nyuzi sita na mumewe baada ya kumkatalia kufanya mapenzi kinyume na maumbile.


Akizungumza leo Alhamisi Februari 14, 2019 mwanamke huyo anadai mume wake amekuwa akimtaka wafanye mapenzi kinyume na maumbile muda mrefu lakini amekuwa akikataa kwa sababu ni haramu kwa mujibu wa mafundisho ya dini.

Akieleza zaidi alidai kwa muda mrefu ndoa yake imeingia kwenye mgogoro na mumewe amekuwa akimwambia kuwa hajui mapenzi.

“Alianza kunitaka kinyume na maumbile miezi mitatu tangu anioe nikamkatalia, mpaka nikapata mimba ikiwa na miezi sababu bado akawa anataka nikamkatalia,” anasema.

Amedai kuwa baada ya kufuatlia historia ya mumuwe, majirani wanaomfahamu walimweleza kuwa tabia hiyo ndiyo imesababisha kuachana na wake zake zaidi ya wawili.

Hata hivyo, mwanaume huyo amekanusha tuhuma hizo na kueleza kuwa mgogoro wa ndoa yake umesababishwa na wakwe zake wanaomdai mahari mpaka imefikia hatua ya kumweleza kuwa ni maskini.

Na Muhammed Khamis, Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527