WATUMISHI WA SERIKALI WALIOFARIKI KWA AJALI YA GARI MTONI WAAGWA




Miili ya wataalam tisa wa idara ya ardhi na idara nyingine za Serikali waliofariki kwa ajali ya gari baada ya kutumbukia Mto Kikwawila , inaagwa leo Februari 25, katika viwanja vya Can, Tangani mjini Ifakara.

Kwenye tukio hilo Viongozi mbali mbali wa serikali wamehudhuria, akiwemo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula, mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe, pamoja na wafanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero na Ifakara.

Ajali hiyo ilitokea Jumamosi ya Februari 23 saa 11 jioni katika Mto Kikwawila baada ya gari aina ya Toyota Land Cruiser Hard Top linalomilikiwa na wilaya ya Kilombero, kutumbukia kwenye mto huo na kusababisha vifo vya watumishi hao wa kitengo cha upimaji ardhi, huku wanne wakijeruhiwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post