Breaking : MWIGULU NCHEMBA APATA AJALI,KAKIMBIZWA DODOMA


 
Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba amepata ajali leo asubuhi Jumatano Februari 13, 2019 katika eneo la Migori mkoani Iringa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amethibitisha waziri huyo wa zamani wa Mambo ya Ndani kupata ajali na kwamba amepelekwa katika hospitali ya Mkapa jijini Dodoma kwa matibabu.

Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dk Alphonce Chandika amesema walimpokea mbunge huyo saa 3:30 asubuhi.

"Alikuwa akilalamika maumivu katika nyonga, mguu wa kulia. Tumempeleka katika vipimo ikiwemo CT Scan," amesema.









Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527