TEKNOLOJIA MPYA KUWASAIDIA VIZIWI KUENDESHA TAXI

Mji mkuu wa Korea Kusini umepata madereva wa kwanza wa teksi viziwi wiki hii, kwa msaada wa teknolojia ambayo imezinduliwa ya kupunguza unyanyapaa wa kuwaajiri watu walio na ulemavu huo.

Kulingana na mtandao wa habari wa Korean Times, dereva wawili viziwi walianza kusafirisha abiria kwenye mji mkuu wiki hii wakisaidiwa na teknolojia iliyoundwa na kampuni mpya ya Coactus.

Akielezea jinsi teknolojia hiyo inafanya kazia mtandao wa Yonhap unasema kuwa vifaa hivyo vimewekwa viti vva mbele na nyuma vya teksi na vimeunganishwa na kampuni kampuni za teksi za Goyohan au silent Taxi.

Teknolojia hiyo inawezesha mawasiliano ya sauti na ujumbe ulioandikwa kuwasaidia abiria kuelezea maeneo wanataka kwenda na mifumo ambayo wangependa kutumia kulipa.

Iliundwa na kundi la wanafunzi mjini humo na kuongozwa na mwanafunzi aliyefuzu na taalumaa ya uandisi Song Min-pyo.Haki miliki ya pichaGOYOHAN TAXIImage captionMkurugenzi mkuu Song Min-pyo

"Tulitaka kuwapa watu viziwi ajira zaidi," Bw Song aliliambia gazeti la Korea Times.

"Tulijua kuwa wakorea watatoka nje ya gari ikiwa dereva ataanza kuwasiliana akitumia simu na kalamu kwa hivyo tukaunda teknolojia hii.'

Yonhap anasema kuwa Coactus itapunguza unyanyapaa unaowakumba madereva visiwi nchini Korea Kusini.

Watu 255,000 wana matatizo ya kusikia nchini Korea Kusini kwa mujibu wa wizara ya afya.
Chanzo : Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post