TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA LEO JUMATANO 16.01.2019

Manchester United wamekubali kumuuza kiungo wao wa kati, mbelgiji Marouane Fellaini, 31, kwa kima cha euro milioni 15 mwezi huu.


Tayari vilabu vya AC Milan, Porto na Guangzhou Evergrande ya Uchina vimeonesha nia ya kutaka kumsajili. (Mirror)

Chelsea wanatarajiwa kuendelea mbeli na mpango wao wa kumsajili mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, ambaye yuko kwa mkopo AC Milan, kufikia mwisho wa wiki hii. (Telegraph)

Meneja wa AC Milan Gennaro Gattuso amesema kuwa Higuain hajamwambia kuwa anataka kuondoka klabu hiyo. (Evening Standard)

Christian Eriksen, 26,huenda akatia saini mkataba mpya na Tottenham, wakati ambapo Real Madrid pia inapigiwa upatu kumsajili kiungo huyo wa kati raia wa Denmark. (AS)

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527