SANAMU LA SHETANI LASHUTUMIWA KUFURAHI SANA

Sanamu la shetani linalopangwa kuwekwa katika mji wa Uhispania Segovia limeshutumiwa kwa kufurahi sana.


Sanamu hilo la shaba bronze liliundwa kwa heshima ya ngano au hadithi ya kale inayosema kuwa shetani alihadaiwa kujenga bomba mashuhuri la maji mjini humo.

Lakini wakaazi wanasema shetani huyo - anayetabasamu na anayeonekana kupiga slefie na simu ya mkononi - anaonekana kuwa na upole na urafiki mwingi.

Msanii huyo ameiambia BBC ameshangazwa na kiwango cha shutuma zilizoelekezwa kwa kazi yake.

Jaji mmoja sasa ameagiza sanamu hilo lisiwekwe kwa sasa wakati anaposhauriana kufahamu iwapo linadhalilisha Wakristo.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527