SAMAKI AUA MTU


Katika mji wa Brooklyn nchini Marekani, kumekumbwa na mkasa wa mama anayedaiwa kupika samaki na harufu iliyotoka, imemuua mwanawe mdogo.

Hadi sasa suala hilo liko katika uchunguzi mikononi mwa mamlaka za kiserikali kupata ukweli wa kifo hicho, kilichoanzia kwa mtoto mhusika mwenye miaka 11 kuugua ghafla, kulegea kwa muda na kupoteza fahamu.

Mtoto Cameron Jean-Pierre, anadaiwa alikuwa na historia ya aleji ya samaki na katika siku ya Mwaka Mpya wiki moja na nusu iliyopita, mama yake alikuwa anaandaa mapishi, harufu ilimfikia mtoto aliyeanguka na kuzimia, mahali hapo anakoishi bibi yake.

Hadi sasa wachunguzi wa kitabibu hawajatoa ufafanuzi kuhusu kilichojiri katika afya ya mtoto huyo ambaye ameshafariki, ingawaje wanafamilia wanakazania chanzo cha kifo hicho ni maradhi ya pumu.

Mama wa mtoto huyo, Jody Pottingr, anasimulia kwamba mwanawe alianza kuugua nyumbani kwa bibi yake, pale binafsi alikuwa alikaanga aina ya samaki hao wa asili.

Mzazi huyo anahisi samaki huyo aliguswa na kitu ambacho kina mtazamo wa sumu kwa samaki wake na ndicho kilicholeta athari inayotajwa na aleji inayotajwa mtoto huyo, iligunduliwa kupitia uchunguzi wa kiafya shuleni, siku moja alivyojisikia vibaya baada ya mlo wa mchana .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post