BODABODA AUAWA KWA KUPIGWA NA ABIRIA KISA KAKATAA NAULI YA 500

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linamsaka mtu mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi kwa tuhuma za kumuua dereva bodaboda Salumu Ramadhan (40).

Tukio hilo lilitokea Jumatatu ya Januari 7, 2019 majira ya saa nne usiku eneo la Foren Pub - Mawenzi katika Manispaa ya Morogoro ambapo mtuhumiwa alimpiga bodaboda huyo kichwani baada ya kukataa kumpakia mwanamke aliyekuwa naye kwenye pikipiki kwa nauli ya Sh500. 

Na Hamida Shariff, Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527