WANAFUNZI 38,842 HAWAKUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA PILI 2018...ANGALIA MATOKEO HAPA

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) Dk Charles Msonde, amesema watahiniwa 506,235 walisajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha pili kati yao wanafunzi 38,842 sawa na asilimia 7.13 hawakufanya mtihani kutokana na ugonjwa na utoro.

Dkt. Msonde ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza matokeo ya kidato cha pili na darasa la nne kwa mwaka 2018, ambapo amesema wanafunzi katika mtihani huo 452,273 sawa na asilimia 89.68 wamefaulu.

Aidha amesema wanafunzi 52,073 wameshindwa kupata alama za kuwawezesha kuendelea na masomo ya kidato cha tatu.

Kuhusiana na matokeo ya darasa la nne kati ya watahiniwa 1,302,461 wa darasa la nne waliofanya mtihani huo sawa na asilimia 95.58, waliofaulu kwa kupata daraja A, B, C, na D ni 1,213,132 sawa na asilimia 93.16.

"Ubora wa ufaulu umezidi kuimarika kwa kuwa watahiniwa waliofaulu kwa daraja A,B na C umeongezeka kwa asilimia 0.03 ikilinganishwa na mwaka 2017,”amesema Dkt. Msonde."

Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa ya Kidato cha Pili (FTNA) 2018 Na Darasa la nne (SFNA) 2018 yametangazwa..Yaangalie hapa

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527