KIJANA MATATANI KWA KUBAKA MBUZI..MWENYEWE ASEMA ALIKUBALIANA NA MBUZI


Pichani, Kennedy Kambani pamoja na mbuzi anayetuhumiwa kumbaka.


Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Kennedy Kambani (21) huko Machinji, Malawi, ameshtakiwa kwa kumbaka mbuzi kwa madai kwamba aliomba ruhusa ya kufanya jambo hilo kwa mnyama huyo kabla ya kumuingilia.

Kamanda wa polisi, Lubrino Kaitano ameeleza kwamba kwa mujibu wa mmiliki wa mnyama huyo Pemphero Mwakhulika, alifikiri Kambani alikuwa akitaka kuiba mbuzi huyo alipomuona awali, lakini alipokwenda kuita watu ndipo alimkuta akifanya ngono na mbuzi wake.

Aidha ameeleza kwamba Kambani alikamatwa na kupelekwa kwenye kituo cha polisi na kushtakiwa kwa kitendo hicho lakini amedai kwamba yeye alimwomba ruhusa mnyama huyo kwanza.

Imeelezwa kwamba Mbuzi huyo alikuwa sehemu ya kundi la malisho kando ya Mchinji lakini jinsia yake haijatajwa.

Matukio ya binadamu kubaka wanyama yamekuwa yakitokea mara kwa mara ambapo Zambia, Sicko Reuben Mwaba,(22), alihukumiwa miaka 15 kwa kubaka mbuzi huku, Feselani Mcube ( 33), wa Afrika Kusini naye akituhumiwa kubaka mbuzi wa jirani yake aliyekuwa mjamzito.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527