MAN UNITED KUUMANA NA CHELSEA MZUNGUKO WA TANO

Mabingwa watetezi wa kombe la FA, Chelsea, wataminyana na mabingwa mara 12 wa kombe hilo, Manchester United, katika mzunguko wa tano wa michuano hiyo.
Mechi ya miamba hiyo itakuwa ni marudio ya fainali ya mwaka jana mabapo Chelsea waliibuka na ushindi.

Timu ya Ligi Daraja la Pili ya Newport County wanaweza kuminyana na mabingwa wa Ligi ya Uingereza Manchester City iwapo watawang'oa Middlesbrough katika mechi yao ya marudiano.

Michezo ya raundi ya tano ya michuano ya FA itapigwa kati ya tarehe 15 na 18 ya mwezi Februari.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527