LUKAKU MAMBO YOTE UNITED

Romelu Lukaku ana jukumu kubwa katika kikosi cha Manchester United, asema meneja wa muda wa klabu hiyo Ole Gunnar Solskjaer.

Lukaku ameanza mechi mara moja tangu Jose Mourinho afutwe kazi kama meneja wa klabu hiyo.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Everton aliyejiunga na Man Utd kwa kima cha pauni milioni 75 amecheza mechi sita za ligi kuu ya England chini ya uongozi wa Solskjaer.

Solskjaer amesifia umahiri wa Rashford, Jesse Lingard na Anthony Martial.

Lakini raia huyo raia huyo wa Norway amesema Lukaku, 25, anasalia kuwa kiungo mhimu wa kikosi chake.

Rashford na Paul Pogba ambao wamefunga zaidi ya mabao matatu yaliyotiwa kimyani na Lukaku tangu Mourinho alipotimuliwa Disemaba 18 mwaka jana.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527