CHINA YAOTESHA PAMBA MWEZINI

Mbegu ambazo zimepelekwa mwezini na chombo cha utafiti wa anga za juu cha Chang'e-4 zimechipua, mamlaka jijini Beijing zimethibitisha.

Hii ni mara ya kwanza kwa mmea wa kibaolojia kuchipuwa mwezini, na ni hatua inayofungua njia ya tafiti zaidi za kisayansi mwezini.

Chang'e 4 pia ndio chombo cha kwanza kutafiti sehemu ya mbali zaidi ya mwezi, ambayo haitazamani na uso wa dunia.

Chombo hicho kilitua mwezini Januari 3 kikiwa kimebeba vifaa vya kuchunguza jiolojia ya eneo hilo.

Mimea imekuwa ikioteshwa kwenye kituo cha kimataifa cha anga za juu lakini haijawahi kujaribiwa mwezini.

Hii inafungua milango ya uwezekano wa wanaanga kuweza kuzalisha chakula chao wenyewe wakiwa anga za mbali na kupunguza uhitaji wa kurudi duniani ili kufuata chakula.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527