CHADEMA WATUMA MAWAKILI KUFUATILIA AFYA YA FREEMAN MBOWE GEREZANI


Chadema imetuma mawakili wake katika Gereza la Segerea kufuatilia afya ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ambaye jana alishindwa kufika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kusikiliza kesi inayomkabili, ikielezwa kuwa ni mgonjwa.

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu jana alisema taarifa za kuumwa kwa Mbowe ambaye pia ni mbunge wa Hai zimewashtua kwa sababu walikuwa hawajui.

Alisema kutokana na taarifa hiyo wamelazimika kuwatuma mawakili kwenda gerezani ili kujua ni kitu gani kinachomsumbua na kujua kama amepatiwa huduma zinazostahili na kama kuna kitu kinachohitajika.

Taarifa za ugonjwa wa Mbowe zilitolewa mahakamani hapo na wakili wa Serikali mwandamizi, Patrick Mwita, wakati kesi ya ya jinai inayomkabili yeye na viongozi wengine wanane wa chama hicho mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ilipotajwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527