CAG AHOJIWA ZAIDI YA SAA TATU DODOMA

Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imetumia zaidi ya saa tatu kumhoji Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG), Prof.Mussa Assad kufuatia wito wa Spika Job Ndugai kumtaka kufika kwenye kamati kutokana na kauli yake ya kuliita bunge dhaifu.

Prof.Assad ameanza kuhojiwa 5:06 asubuhi na mahojiano yake yalihitimishwa saa 8:47 mchana.

Awali baada ya kuingia kwenye ukumbi Prof.Assad alitoka nje ya ukumbi saa 6:45 mchana akisubiri kamati ikijadili hoja zake na mwenendo wa mahojiano ili kama kuna haja ya kufafanua aitwe tena.

Baadate ameitwa saa 7:15 mchana na kutoka 7:57 mchana ambapo alikaa kwa muda kusubiri kuitwa tena saa 8:35 mchana kuelezwa uamuzi wa shauri lake.

Kamati hiyo ilimaliza mahojiano naye saa 8:47 mchana chini ya Mwenyekiti wake Emmanuel Mwakasaka.


“CAG Prof. Assad amefika leo mbele ya kamati baada ya wito aliopewa na Spika na tumemhoji. Sisi kwa kanuni zetu hapa tunamwita mtuhumiwa, tukishakamilisha hili suala tunalipeleka kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai,” amesema Mwakasaka.

Aidha, Mwakasaka amesema Prof. Assad ameonyesha ushirikiano mkubwa kwa maswali aliyoulizwa kamati hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527