KATIBU MKUU WA CCM : VYAMA VINAVYOTAFUTA WAFUASI MITANDAONI,MAHAKAMANI VITAKUFA




Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi nchini Tanzania Dkt. Bashiru Ally amesema vyama vinavyotafuta wafuasi kwenye nyumba za ibada,mahakamani,mitandaoni safari yao siyo ndefu vitakufa kifo cha mende.

Dkt. Bashiru ameyasema hayo leo Jumatatu Januari 7,2018 wakati akizungumza na wanachama wa CCM mkoa wa Shinyanga katika ukumbi wa CCM mkoa wa Shinyanga.

Amesema kutokana na vyama vya siasa kutafuta wafuasi kwenye misikiti,makanisa,mahakamani na mitandaoni haviwezi kufika mbali basi vitakufa kwa sababu ya kujitakia wao wenyewe.

Ameviomba vyama vya siasa kutoshinda mahakamani kutafuta ruzuku na kwamba wanahitaji ushindani wa kweli wa maendeleo. 

“Tunahitaji kujenga chama kwa misingi ya kidemokrasia,tunataka ushindani utawavutia watanzania kuendelea kutuamini,Kadri tutakavyojiimarisha tutakuwa chama mfano kwa vyama vingine 

Aidha amewataka wanachama wa CCM kuacha tabia ya kutafuta ubunge na nafasi zingine za uongozi na badala yake wawaache viongozi waliochaguliwa watekelezea majukumu yao na muda utakapofika wa kufanya uchaguzi. 

Na Kadama Malunde- Malunde1 blog
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi nchini Tanzania Dkt. Bashiru Ally  akizungumza na wanachama wa CCM katika ukumbi wa CCM mkoa wa Shinyanga leo - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527