MAMA KARUME ANENA 'SERIKALI NI MAKINI TUIPENDE TUSITAKE KUIFITINISHA NA YANGA'

Mjumbe wa Baraza la wadhamini la klabu ya Yanga, Mama Fatma Karume amewataka viongozi wa Yanga kuahakikisha wanafanya uchaguzi bila kuiogmbanisha Yanga na serikali kwa maslahi yao binafsi.

Akiongea na baadhi ya wanachama wa Yanga kuhusu mwenendo wa klabu hiyo, Mama Fatma Karume alieleza kushangazwa na maneno yanayoenezwa kuwa huenda uchaguzi wao unakwamishwa na serikali kupitia BMT jambo ambalo si kweli.

''Hizi chokochoko zinatoka wapi, mara uchaguzi usifanyike kwa kusingizia serikali inaingilia, niwaombe tufanye uchaguzi vizuri hawa viongozi wenye kuigombanisha Yanga na serikali hatuwahitaji'' , amesema.

Mbali na hilo Mama Fatma amewahakikishia wanachama wa Yanga kuwa serikali haiwezi kuingilia uchaguzi wao endapo watafuata taratibu zote kwa mujibu wa sheria na katiba ya klabu hiyo pamoja na maelekezo mengine kutoka TFF na mamlaka zinazohusika.

''Serikali yetu ni makini na inasimamia kila lililojema, kwahiyo tuipende na tusitake kuifitinisha na Yanga, Yanga tunaipenda na serikali yetu tunaipenda tufuate taratibu ili timu yetu ipate viongozi wanaofaa'', ameongeza.

Yanga ipo kwenye sintofahamu juu ya suala la uchaguzi wao ambao unasimamiwa na kamati ya uchaguzi ya TFF lakini wao kama klabu wamekuwa wakishinikiza uchaguzi huo usiguse nafasi ya mwenyekiti jambo ambalo TFF hawaliungi mkono.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527