WANAJESHI WALIOANDAMANA KWENDA KWA WAZIRI MKUU WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA

Mahakama ya jeshi nchini Ethiopia imewahukumu wanajeshi 66 kati ya miaka 5 na 14 kwa kuandamana kwenda ikulu ya waziri mkuu Abiy Amhed mwezi Oktoba mwaka huu na kwa kuvunja kanuni za jeshi, kwa mujibu wa maafisa.

Wanajeshi hao 66 walikuwa miongoni mwa wanajeshi 200 waliokuwa wamevaa sare ambao walifika wakiwa wamejihami kwenye majengo ya ikulu ya Abiy tarehe 10 Oktoba katika kile serikali ilisema lilikuwa ni shinikizo na kutaka waongezewe mshahara.

Lakini Abiy ambaye alionyeshwa kwenye televisheni akifanya mazoezi na wanajeshi hao alisema viongozi wao walikuwa na nia ya kusitisha mabadiliko nchini humo na wanajeshi ambao hawakutajwa majina walisema walijutia kupoteza fursa ya kumuua Abiy.

Kanali Meshesha Areda, mkuu wa mahakama za kijeshi aliwaambia waandishi wa habari kuwa mahakama ya jeshi ilimhukumu mwanajeshi mmoja miaka 14 na wengine 65 kati ya miaka 5 na 13 kwa kukiuka kanuni za jeshi.


Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527