MWANAUME AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI

Mwanamume aliyeuawa kimakosa jimboni Alabama, Marekani ameuawa kwa kupigwa risasi mara tatu kutoka nyuma, uchunguzi wa maiti yake umebaini.


Emantic Bradford Jr, anayefahamika kama EJ, alipigwa risasi kichwani, shingoni, na kwenye mfupa wa nyonga akiwa katika jumba la kibiashara la Riverchase Galleria mjini Hoover, Alabama.

Polisi walikuwa wamedhania yeye ndiye mshambuliaji aliyewaua watu wawili kwa kuwapiga risasi - mwanamume mmoja wa miaka 18 na msichana wa miaka 12 mwezi jana.

Lakini baadaye polisi walikisi kwamba walikuwa wamekosea, na sasa wamemkamata mwanamume mwingine wanayesema ndiye mshukiwa halisi.

Mwanamume huyo anayezuiliwa kwa sasa, Erron Brown, 20, alijisalimisha mwenyewe kwa polisi.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527