NDEGE MPYA AIRBUS A220-300 KUTUA TANZANIA JUMAPILI HII

Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas amesema Serikali itapokea ndege yake nyingine mpya toleo la Airbus A220-300 Jumapili Desemba 23, 2018.

Abbas ameeleza hayo leo Ijumaa Desemba 21, 2018 katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter.

“Ungana nasi kuipokea ndege ya kwanza kununuliwa na Serikali kwa toleo la Airbus A220-300. Ni Tanzania pekee.’Ngorongoro-Hapa kazi Tu’, itawasili nchini Jumapili hii na siku chache baadaye ndege nyingine kama hiyo itawasili Dodoma-Hapa Kazi Tu,” ameandika Dk Abbas.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527