Miss Tanzania:NIPO KWENYE NAFASI NZURI , NAHITAJI KURA ZA WATANZANIA KUWA MSHINDI

Zikiwa zimebaki siku mbili ili kufanyika kwa kilele cha shindano la urembo la dunia (Miss World), mwakilishi wa Tanzania, Queen Elizabeth Makune, ameendelea kuwa nafasi za juu huku Watanzania wakihimizwa kumpigia kura kwa wingi ili ashinde.

Queen Elizabeth ambaye yupo Sanya China tayari kwa mashindano hayo yanayojumuisha warembo zaidi ya 50 kutoka nchi mbalimbali duniani, amesema bado anahitaji kura ili aweze kutwaa taji hilo.

“Naomba Watanzania wenzangu pamoja na wadau wa urembo wanipigie kura ili niweze kuingia katika nafasi ya ushindi ili kupeperusha vyema bendera yetu, mpaka sasa nipo katika nafasi nzuri,” alisema Queen.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527