MANARA ATUMA SALAMU KWA MWANA FA


Ikiwa imepita siku moja tu ,tangu klabu ya Simba kupata matokeo mabaya ya kufungwa jumla ya mabao 3 – 2 dhidi ya Mashujaa FC na kuyaaga mashindo ya Azam Sports Federation Cup (FA), mapema hii leo Afisa habari wake, Haji Manara ameonyesha gari jipya aina ya Ferrari huku akielezea kuwa msemaji mkubwa ndiye mwenye hadhi ya kutumia.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Manara ameweka picha ya gari jipya aina ya Ferrari huku akiandika gari hilo ndio hadhi ya msemaji mkubwa mwenye ustaa wake.

”Engineer @mwanafa soma hyo!!, Yajayo ndio hayo madhee!!, Ferrari ndio hadhi ya msemaji mkubwa mwenye wastawa wakemjini!!, No Nzi wala lift,Dadadeki,” ameandika Manara kwenye mtando wake wa Instagram

Mkuu huyo wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba SC, Haji Manara ameonekana kwenye gari hiyo ya Ferrari ya rangi nyekundu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527