DROO YA AFCON KUPANGWA LEO DAR


Droo ya upangaji wa makundi ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 (AFCON) inatarajiwa kupangwa hii leo Jijini Dar es salaam.

Upangaji wa droo hiyo utafanyikia kuanzia saa 1:00 usiku katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, ukiratibiwa na Shirikisho la Soka barani Afrika CAF na Shirikisho la Soka Tanzania TFF ambao ndiyo wenyeji wa michuano hiyo.

Timu zilizofuzu kushiriki michuano hiyo ni pamoja na Mwenyeji, Tanzania, Angola, Cameroon, Guinea, Morocco, Nigeria, Senegal and Uganda.

Fainali za michuano hiyo zinatarajia kufanyika kuanzia Aprili 14 hadi 28, 2019 ambapo timu zitakazofuzu hatua ya nusu fainali, zitaliwakilisha bara la Afrika katika michuano ya Dunia ya vijana chini ya miaka 17 itakayofanyika mwakani nchini Peru.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527