SANCHEZ MATATANI UNITED,ZIMWI LA MOURINHO LAMVAA

Mshambuliaji wa Chile Alexis Sanchez, 29, anataka sana kuihama Manchester United baada yake kuanza kupuuzwa na meneja Jose Mourinho. (Mirror)

Juventus na Inter Milan wanahusishwa na kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Tottenham na Ubelgiji Mousa Dembele, 31, ambaye mkataba wake katika klabu yake ya sasa utafikia kikomo mwisho wa msimu huu. (Calciomercato)


Newcastle wameongeza juhudi zao za kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Paraguay anayechezea Atlanta United Miguel Almiron, 24. (Mail)

Bayern Munich wanapanga kuwasilisha ombi la kumnunua mchezaji anayeng'aa sana akichezea timu ya taifa ya England ya vijana wasiozidi miaka 17 Callum Hudson-Odoi, 18 anayechezea Chelsea kwa sasa mwezi Januari. (Sun)

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527