Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa anatarajia kufanya ziara ya siku nne mkoani Kagera ambapo atazindua miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu na afya katika wilaya za Kyerwa,Bukoba,Muleba na Biharamulo Karagwe sambamba na kuongea na wananchi katika mkutano wa adhara mjini Bukoba.
Akitoa taatifa hiyo kwa waandishi wa habari leo asubuhi ofisini kwake, Mkuu wa mkoa wa Kagera brigedia jenerali Marco Gaguti amesema waziri mkuu atawasili mkoani Kagera Oktoba 6 ambapo anatarajiwa kuhitimisha ziara yake Oktoba 9 mwaka huu.
Na Angela Sebastian- Malunde1 blog
Download/Pakua App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527