MWANAFUNZI AUAWA KWA KUCHOMWA KITU CHENYE NCHA KALI

Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Jumbi, Sabra Ussi Khamis amefariki dunia baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali na mtu anayedaiwa kuwa mgonjwa wa akili.


Tukio la kuuawa kwa binti huyo limetokea jana Oktoba 2, 2018 majira ya saa mbili usiku wakati Sabra alipokuwa akiuza duka nyumbani kwao na ghafla alitokea kijana huyo anayesadikiwa kuwa mgonjwa wa akili Hafidh Mkubwa Suleiman (21) na kumchoma na kitu tumboni.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Thobias Sedeyoka amesema ni kweli tukio hilo limetokea na wanaendelea na uchunguzi kubaini taarifa zaidi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527