MO DEWJI : NAFURAHI KUONA MAONO YANGU YANAKAMILIKA..HATA SIKU NISIPOKUWEPO DUNIANI....

Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Mo Dewji amewahakikishia mashabiki wa klabu ya Simba kuwa Uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo utakamilika kama alivyopanga ili kutimiza ahadi yake.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Mo Dewji amesema anafanya hivyo kumalizia ujenzi wa uwanja huo ili utumike hata kama yeye asipokuwepo duniani.

“Tumefika hatua nzuri ya maendeleo ya uwanja wetu wa mazoezi wa #SIMBA. Nafurahi kuona maono yangu yanakamilika ili hata siku nisipokuwepo duniani, uwanja uendelee kutumika kwa mazoezi Insha’Allah.” ameandika MO.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527